Mashirika ya kutetea haki za watoto yanalaumu serikali ya nchi hiyo, kwa kutochukua hatua madhubuti dhidi ya mashirika ya kuchimba madini yanayoajiri watoto hasa katika mikoa ya kivu ya kaskazini na Kivu ya Kusini.
Jimbo la Kivu Kusini ni moja ya maeneo yenye utajiri mkubwa wa madini ambapo idadi kubwa ya watoto wanafanya kazi ya uchimbaji katika migodi. Ripota wetu BYOBE MALENGA alitembelea mji wa Kamituga ,na kushuhudia hali ilivyo na hii hapa taarifa yake.
Share





