Swala la wakimbizi na wahamiaji limekuwa linakuna vichwa vya viongozi duniani. Hivi karibuni, viongozi wa dunia walikutana mjini New York Marekani katika kongamano la Umoja wa Mataifa kuangazia maswala ya wakimbizi na wahamiaji.
Imedhihirika wazi kuwa msaada kwa wakimbizi umekuwa unapungua siku hadi siku.
Mataifa tajiri yamehimizwa kuchangia pakubwa ili kustaawisha wakimbizi walioko katika nchi zinazoendelea na zile zenye migogoro.
Muandishi wetu wa Burundi Ramadhani KIBUGA ametembelea kambi ya Kavumu ikiwa ni moja ya kambi za wakimbizi wa Jamhuri ya Kidemokaria ya Congo ilioko mashariki mwa Burundi katika mkoa wa Cankuzo nakuzungumza na baadhi ya wakimbizi wanao ishi kambini humo.
Share





