Wanafunzi wata anza kurejea darasani katika majimbo ya mashariki ya Australia, kuanzia wiki ijayo hali ambayo inamaanisha kurejea kwa msongamano barabarani tena.
Katika majimbo ya Queensland na New South Wales, wanafunzi wote wa shule za umma watarejea darasani.
Ilhali jimboni Victoria, jimbo ambalo limevumilia shinikizo nyingi kwa muda mrefu, kurejea kwa wanafunzi darasani kutakuwa kwa utaratibu.
Na unaweza endelea kupata taarifa mpya kuhusu coronavirus, katika lugha yako kwenye tovuti ya: sbs.com.au/coronavirus
Share






