Ripoti ya mwisho kuhusu mabadiliko yaliyopendekezwa na Serikali kwa Mpango wa Kitaifa wa Bima ya Ulemavu itawasilishwa Bungeni leo. Uchunguzi huo ulizinduliwa katika mwezi Mei ili kuchunguza mapendekezo ya Serikali, ya kuokoa karibu dola bilioni 38 kwa kipindi cha miaka minne.
Sikiliza makala yetu yaliyo rekodiwa hapa
Mchunguzi wa usalama wa usafiri anasema uchunguzi ulianzishwa mara moja mara tu alipopokea taarifa ya tukio la tatu la njia ya ndege kurukia, katika Uwanja wa Ndege wa Sydney lililohusisha ndege mbili, katika wiki mbili zilizopita. Ofisi hiyo inasema wadhibiti wa trafiki wa ndege walighairi kibali cha kupaa kwa ndege ya Virgin Australia, wakati huo huo wafanyakazi wake walipoona ndege ya Qantas ikianza kuvuka njia ya kurukia ndege iliyo mbele yao.
Nchini Kenya, uwepo wa wanajeshi wa Uingereza karibu na Nanyuki katikati mwa Kenya unaendelea kuzua mijadala. London ina kambi ya mafunzo ya kijeshi huko, BATUK.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.






