Wazazi wangu walikutana gerezani, na gereza lilikuwa jambo la kawaida wakati nilikuwa nikikua. Kisha, mlipofikia wakati wangu wa kwenda gerezani, nilikuwa nimekamilisha kifungo cha mara nyingi sana, hata siwezi kuhesabuRocket Bretherton
Huyo ni Rocket Bretherton - mwanamke wa jamii ya Noongar aliyekulia katika mazingira ya madawa ya kulevya na unyanyasaji wa majumbani na alienda jela kwa mara ya kwanza akiwa na umri wa miaka 15. Siku hizi, yeye ni mpiga sauti anayeshinda tuzo nyingi, mzungumzaji na mpiganaji wa mabadiliko - ambaye amekuwa akifanya kazi na Tume ya Marekebisho ya Sheria kwa zaidi ya miaka mitatu. Rocket anasema alihudumia hukumu kama 30 kote Queensland na Northern Territory.
Nilikuwa nikisubiri kurudi jela. Nilijua siku hiyo itafika. Nilikuwa nikiuza dawa za kulevya ili kujikimu, na nilijua kwamba nilichokuwa nikifanya, na kile ambacho ningekamatwa nacho, kingenipeleka jela, lakini sikuwa na wasiwasi sana kwa sababu kwa namna fulani nilitarajia kurudi jela kwa mapumziko kidogo.Rocket
Haikuwa rahisi kuvunja au kuacha tabia hiyo.
Nilijaribu mara nyingi kuacha dawa za kulevya nilipotoka jela, lakini hakuna msaada kabisa. Mnapotoka jela, mnaachwa tu mlangoni, na kama mmekuwa na kifungo kilichositishwa, mnaachwa kwenye idara ya marekebishoRocket
Masharti ya marejeleo yatatoa fursa kwa uchunguzi kuchunguza iwapo haki za watoto zinakiukwa, na jinsi hili linavyolingana na majukumu ya Australia chini ya sheria za kimataifa.
Madai ya unyanyasaji, matumizi ya vizuizi kama vile vifungi vya mdomo, na masuala ya msongamano pamoja na jukumu la mipango ya kirekebisho na mwelekeo ,yanategemewa kuwa kipaumbele muhimu.
Kamishna wa Kitaifa wa Watoto anayemaliza muda wake, Anne Hollonds, anasema mifumo ya haki ya vijana na vizuizi vinaonyesha baadhi ya masuala makubwa zaidi ya haki za binadamu nchini leo.
[Tunaongelea Watoto walio hatarini zaidi nchini. Hawa ni watoto wanaokabiliana na matatizo makubwa, masuala ya afya ya akili, ulemavu wa maendeleo, matatizo ya kujifunza, na mshtuko. Wanaathiriwa na madhara wao wenyewe na pia ni wahanga wa uhalifu wao wenyewe.Bi Hollonds
Bi. Hollonds aliwasilisha ripoti kubwa juu ya mifumo ya haki kwa vijana mnamo Agosti mwaka jana. Iligundua kuwa sera za serikali za majimbo zinazodaiwa kuwa kali dhidi ya uhalifu hazijatokana na ushahidi, na haziwezi kupunguza uhalifu.
Bi. Hollonds anasema kwamba uwekezaji katika mifumo ya kuzuia - kama vile elimu, makazi, afya na ulinzi wa watoto - ndiyo ufunguo wa kupunguza wimbi la uhalifu miongoni mwa vijana.
Swali linaweza kuulizwa, Je, inahitaji nini kuchukua hatua juu ya ushahidi? Tulichokiona ni kwamba tunakwepa majukumu yetu kwa watoto hawa mpaka wafanye kosa, kisha tunawaadhibu kwa ukali kwa njia ambazo nchi zingine hazifanyi hivyoAnne Hollonds
Ripoti yake ilipendekeza serikali ya shirikisho iingilie kati na kuanzisha kikosi kazi cha kitaifa, pamoja na waziri anayehusika na ustawi wa watoto. Alipendekeza pia viwango vya chini vya kitaifa vinavyoweza kutekelezwa, ambavyo vitaweka kiwango cha chini kinachokubalika cha huduma - na ambavyo vitaangaziwa na uchunguzi.
Huu ni uchunguzi wa kihistoria unaochunguza tatizo kubwa linalovuka mipaka yote ya shirikisho. Hii ni dharura ya kitaifa.Anne Hollonds
Uchunguzi wa awali kuhusu haki za vijana tayari ulikuwa umezingatia ripoti ya Bi Hollonds - lakini kazi yake ilikatizwa na uchaguzi wa shirikisho. Uchunguzi huo ulikuwa ukiongozwa na Seneta wa chama cha Liberal, Paul Scarr.
Ushahidi tuliopokea ulikuwa muhimu na wenye kusikitisha sana, na tulipokea maoni kutoka kwa zaidi ya wana hisa mia mbiliPaul Scarr
Matumizi yasiyofaa ya kufunga Watoto pekeyao yalikuwa ni masuala muhimu, pamoja na idadi ya watoto waliokuwa kizuizini ambao hawajahukumiwa au wanatarajia kusikilizwa kesi yao ya kwanza mahakamani.
Zaidi ya robo tatu ya watoto walioko kizuizini wanasubiri kesi, na idadi hiyo imeongezeka kwa takriban asilimia 10 katika miaka michache iliyopita. Na kati ya idadi hiyo ya takriban watoto 800, kuna idadi isiyo ya usawa ya watoto wa Mataifa ya Kwanza. Tunazungumzia kuhusu asilimia 60Paul Scarr
Seneta Shoebridge anasema mfumo unashindwa.
Na hatudhani kwamba mnaweza kutoka kuskia data kuhusu viwango vya kifungo vya watu wa Mataifa ya Kwanza kote nchini , na msifikiri kwamba ni mfumo wa kibaguzi unaolenga vijana wa Mataifa ya Kwanza kwa undani.Senator Shoebridge
Mapema mwezi huu, Waziri wa Wenyeji wa Australia, Malarndirri McCarthy, alionyesha wasiwasi wake kuhusu viwango vya juu vya kufungwa kwa watu wa Mataifa ya Kwanza - hasa vijana.
Aliwaambia Seneti kwamba serikali inachunguza wazo la kutumia ufadhili wa shirikisho ili kuzisukuma serikali za majimbo na maeneo kufikia malengo chini ya Mkataba wa Kitaifa wa Kufunga Pengo. Kuzidishwa kwa uwakilishi katika mfumo wa haki za jinai ni mojawapo ya malengo 17.
inasikitisha kujaribu kuwasiliana na majimbo na maeneo kuhusu kufuata makubaliano. Hakuna adhabu katika makubaliano hayo. Na kile ninachojaribu kufanya sasa ni kuangalia mipango ya ufadhili wa shirikisho ambayo imesainiwa na kila jimbo na eneo, juu ya jinsi makubaliano yalivyo, ili kuona jinsi tunavyoweza kuingiza adhabu kuhusiana na kwanini hamfiki malengo hayaMalandirri Mcarthy
Kwa watu wa Kiasili kama Rocket, ushahidi unaonyesha kuwa kukutana mapema na mfumo wa haki mara nyingi kunaweza kusababisha makosa zaidi.
Tayari mnapaswa kujiuliza, kwa nini tumejikita kwenye mfumo huu ambao haufanyi kazi. Tunajua kwamba mtu anapopelekwa jela akiwa mchanga, kuna uwezekano mkubwa wa kuendelea kuhusiana na mfumo wa haki. kile tunachofanya kwa sasa hakifanyi kazi, Tunahitaji kuangalia mambo mengineRocket
Rocket anasema alianza kubadilisha maisha yake alipohisi kuthaminiwa na kusikilizwa. Mpango ndani ya gereza ulimruhusu kutengeneza podikasti akiwa bado humo.
watu wengi walianza kusema: 'Oh Mungu wangu, siwezi kuamini maisha mliyoishi'. Nadhani nilikua nikifikiria kuwa kile nilichopitia nikiwa mtoto kilikuwa cha kawaida, na kila mtu alipaswa kupitia hiloRocket Bretherton
Rocket pia alipokea ziara kutoka kwa mwanasheria wa Arrernte[arr-uhn-duh] Leanne Liddle, alipokuwa akiandaa Makubaliano ya Haki za Wenyeji wa Northern Territory, na akaombwa kutoa ushauri wake.
Mimi kimsingi nilisema inahitaji kuwa kama mpango wa miezi sita. Inahitaji kuwa mbadala wa gerezani, na inahitaji kuwa msaada wa kina. Mnahitaji kupata msaada kwa ajili ya majeraha yenu, mnahitaji kufanya masomo ya unyanyasaji wa kinyumbani na wa kifamilia. Mnahitaji kuwa na uwezo wa kusoma - ikiwa mnataka kusoma. Mnahitaji kuwa na uwezo wa kujiandaa kwa ajili ya kazi. Mnahitaji kuwa na uwezo wa kushughulikia kile kilichowafanya mkose, ambacho kinaweza kuwa ni tatizo la dawa za kulevya na pombe. Lakini pia kuna maswala mengine chini mnajua, ambayo yalisababisha tatizo la dawa za kulevya na pombeLeanne Liddle
Kulingana na masharti yake ya marejeo, uchunguzi wa Seneti umeelekezwa mahususi kutafuta maoni kutoka kwa watu waliopitia mfumo wa haki kwa vijana - na kutafuta njia mbadala zenye ufanisi kwa mbinu ya sasa.
Uchunguzi huu unapokea michango iliyoandikwa hadi tarehe 19-12-2023 - na unatarajiwa kutoa ripoti ifikapo Machi mwaka ujao.







