Watch FIFA World Cup 2026™ LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari: Waziri Mkuu aeleza timu ya soka ya wanawake ya Iran, "msaada upo kama wana uhitaji"

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS / SBS Swahili

Waziri Mkuu wa Australia amesema serikali itamsaidia yeyote kati ya timu ya soka ya wanawake ya Iran ambaye bado hajaomba hifadhi hapa.


Wachezaji watano wamepewa visa za kibinadamu na Serikali ya Australia asubuhi ya leo Jumanne, baada ya kuchukuliwa chini ya ulinzi wa Polisi wa Shirikisho la Australia.

Takriban watu 700 katika Eneo la Kaskazini wako katika makazi ya dharura kufuatia mafuriko makubwa, huku mji wa Katherine bado ukiwa chini ya onyo la mafuriko ya dharura. Takriban watu 1000 wamehamishwa kutoka eneo hilo katika siku za hivi karibuni. Tahadhari pia zipo kwa sehemu kubwa za Queensland, ikiwa ni pamoja na Brisbane, baada ya kupungua kwa joto ya kitropiki kusababisha mafuriko hatari na kuongezeka kwa kasi kwa kina cha mito.

Nchini kenya idadi ya waliofariki kutokana na mafuriko yaliosababishwa na mvua kubwa wiki iliopita, imeongezeka kutoka 23 na sasa idadi hiyo imefikia watu 45, kwa mujibu wa taarifa ya polisi nchini humo. Mbali na idadi ya vifo kuongezeka, idara ya polisi nchini humo imesema waru wapatao 2224 pia walilazimika kuyahama makazi yao, bila hata hivyo kutoa maelezo zaidi.

Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now