Serikali ya Shirikisho inasema vyuo vikuu vinaweza kukabiliwa na faini ikiwa vitashindwa kupambana na ubaguzi wa rangi chini ya viwango vipya vilivyoanzishwa Jumatatu 13 Julai 2026.
Sikiliza makala yetu yaliyo rekodiwa hapa
Mabadiliko hayo yanahitaji taasisi za elimu ya juu kupitisha ufafanuzi wa ubaguzi wa rangi, ikiwa ni pamoja na chuki dhidi ya Wayahudi, chuki dhidi ya Uislamu na ubaguzi wa rangi dhidi yawa Aboriginal na wakaazi wa Visiwa vya Torres Strait.
Polisi wa Shirikisho la Australia wamefichua kuwa zaidi ya familia 120 za watoto waliotambuliwa kama waathiriwa wa unyanyasaji na mfanyakazi wa huduma ya watoto wamewasiliana nao.AFP inasema mshtakiwa anayedaiwa ni mwanaume mwenye umri wa miaka 35 ambaye ameshtakiwa kwa makosa zaidi ya 300 yaliyofanywa kwa kipindi cha miaka 16.
Waasi wa AFC/M23 nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo wametumia mripuko wa ebola katika eneo wanalolidhibiti kuonyesha uwezo wao wa kuongoza nchi. Wamefanya hivyo kwa kuonyesha uwezo wao wa kuongoza nchi kwa kuanzisha juhudi za kukabiliana na mripuko huo tofauti za zile zinazoendeshwa na serikali ya Kinshasa.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.






