Serikali ya taifa yasema iko tayari kwa utoaji wa chanjo za coronavirus

Mtu afanyiwa kipimo cha coronavirus, katika kituo cha vipimo cha fukwe ya Bondi Beach.

Mtu afanyiwa kipimo cha coronavirus, katika kituo cha vipimo cha fukwe ya Bondi Beach. Source: AAP

Serikali ya shirikisho imetangaza kuwa vyeti vitatolewa, kwa watu ambao watakuwa wame chanjwa, iwapo thibitisho itahitajika kwa ajili ya safari au kazi.


Taarifa hiyo imejiri wakati Australia imeripoti siku nyingine, yakutokuwa na visa vyovyote vya maambukizi katika jamii.

Na jimboni Victoria, hapakuwa kesi zozote mpya kwa siku ya tatu mfululizo ila, mamlaka huko wame kiri kuwa huenda hawataweza baini jinsi mfanyakazi katika hoteli ya karantini alivyo ambukizwa virusi hivyo. Mamlaka husika wanafanya tathmini ya vifaa vyakusambaza hewa ndani ya hoteli zote za karantini jimboni Victoria, pamoja na kinga za sura ambazo nilazima zivaliwe na wafanyakazi.

Kwa hatua za afya na msaada ambazo zimewekwa, katika jibu la janga la COVID-19 katika lugha yako, tembelea tovuti hii: sbs.com.au/coronavirus


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now