Taarifa ya habari 11 Mei 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Uwekezaji kwa wanawake, huduma yamalezi yawatoto, huduma ya uzeeni, ulemavu na afya ya akili watarajiwa kuwa sehemu kubwa ya bajeti ya taifa


Mamlaka wa afya wa Kusini Australia wanachunguza kama, mwanaume kutoka Victoria aliyepatwa na virusi vya COVID-19 baada yakumaliza muda wa karantini ndani ya hoteli mjini Adelaide, kama alipata virusi hivyo hapo.

Mwanaume huyo alirejea nyumbani kwake katika kitongoji cha Wollert ambacho kiko kaskazini mwa Melbourne tarehe 4 Mei, nakuanza kupata dalili za ugonjwa huo siku nne baadae, kabla yakupatwa na virusi hivyo jana jumatatu tarehe 10 Mei.

Mawakili wanaomwakilisha mshukiwa wa ufadhili wa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 nchini Rwanda, wameomba mashtaka dhidi yake yaondolewe, kwa madai kuwa hayuko katika hali nzuri kiafya kuweza kuendelea na kesi hiyo. Félicien Kabuga, mwenye umri wa miaka 84, alikamatwa mwaka mmoja uliopita nchini Ufaransa, na anazuiliwa mjini The Hague, Uholanzi, akisubiri kesi kuendeshwa katika mahakama, iliyo nchini Tanzania, inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service