Taarifa ya Habari 27 Juni 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Mkutano wa dharura wa kamati ya usalama wa Australia, utafanywa kesho Jumatatu 28 Juni 2021, kujadili milipuko ya COVID-19 nchini.


Serikali ya jimbo la Kusini Australia imesema inachukua uamuzi thabiti kuzuia usambaaji wa COVID-19, kwakufunga mipaka yake na Queensland, Magharibi Australia, Wilaya ya kaskazini na Australian Capital Territory maramoja.

Ni wakaaji tu wa kusini Australia na wasafiri muhimu, ndiwo watakao ruhusiwa kuingia katika jimbo la Kusini Australia kutoka maeneo hayo. Wakaaji wa New South Wales wanaendelea kupigwa marufuku kuingia jimboni humo, na wakaaji wa Victoria kwa sasa watahitaji kufanyiwa vipimo vya virusi hivyo siku yakwanza wanapo wasili jimboni humo.

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema Ijumaa wimbi la tatu la maambukizi ya virusi vya corona limeikumba taifa na kwamba wagonjwa wa COVID-19 wapo. Rais ametumia nafasi hiyo pia kuwaomba viongozi wa dini nchini kutoa elimu ya kujikinga kwa waumini wao, ikiwemo kusisitiza wachukue tahadhari na kufuata ushauri unaotolewa na wataalam wa afya.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service