Taarifa ya habari 4 Oktoba 2020

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Mweka hazina wa taifa Josh Frydenberg amesema changamoto kubwa inayo kabili uchumi, inahitaji msaada mkubwa, kupiga jeki shughuli pamoja nakukuza ajira.


Rais wa Marekani Donald Trump amesema siku zijazo zitakuwa "mtihani halisi" katika kupona kwake mambukizi ya virusi vya corona, katika ujumbe wa vidio alioweka katika ukurasa wa Twitter siku ya Jumamosi,(03.10.2020).

Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Chadema, Tundu Lissu amesimamishwa kufanya kampeni kwa muda wa wiki moja, kwa shutuma za kukiuka kanuni za uchaguzi. Hatua hiyo imechukuliwa mapema hii Ijumaa na Kamati ya Maadili ya Taifa ya Tume ya Uchaguzi. Katika taarifa yake, kamati hiyo ikisema imechukuwa hatua hiyo kutokana na malalamiko yaliyowasilishwa na Chama cha NRA na CCM.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now