Taarifa ya Habari 5 Agosti 2025

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS / SBS Swahili

Waziri wa mambo ya nje Penny Wong ame muhamasisha Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, asikize wito wakisitisha vita mara moja Gaza.


Jibu la serikali ya Wilaya ya Kaskazini kwa uhalifu wa vijana, limejadiliwa katika tamasha ya Garma ya mwaka huu. Viongozi wa jamii walizungumza kuhusu mfumo wa kizuizi wa vijana katika wilaya ya Kaskazini na, wameiomba serikali ya shirikisho iingilie kati na isitishe hatua za haki ambazo zime undwa kukabiliana na uhalifu wa vijana.

Rais wa DR Congo Félix Tshisekedi anaripotiwa kuwa anakaribia kutangaza mabadiliko ya baraza la mawaziri. Jumamosi, Agosti 2, alithibitisha nia yake kwa viongozi wa Muungano Mtakatifu, jukwaa lake la kisiasa. Tangazo lingine: serikali itapunguzwa. Itapunguzwa hadi chini ya wajumbe 50, ikilinganishwa na 54 wa sasa.

Miaka mitano ya uhai wa bunge la 12 la Tanzania, ulitamatika Jumapili ya wikendi iliopita kufuatia tangazo la rais Samia Suluhu Hassan, kulivunja bunge hilo kwa mujibu wa katiba.
Kuvunjwa kwa bunge hilo kunafungua ukurasa mwingine kwa vyama vya siasa kuanza kuteua wagombea wa nafasi za ubunge kuelekea uchaguzi wa Oktoba 29 mwaka huu.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 5 Agosti 2025 | SBS Swahili