Wanafamilia na Waziri Mkuu Anthony Albanese wamemkumbuka Richard Scolyer, mshindi wa zamani wa tuzo yamu Australia bora wa mwaka.
Mtafiti huyo wa saratani amefariki akiwa na umri wa miaka 59, baada ya kupambana na saratani kali ya ubongo kwa miaka mitatu.
Jeshi la Nigeria limesema leo kuwa limewaokoa watu 360 waliotekwa nyara na kundi la Boko Haram katika eneo la kusini mwa jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi hilo, operesheni hiyo ilifanyika katika Milima ya Mandara, ambayo ni sehemu ya ngome ya kundi hilo la wanamgambo.
Mshambulizi wa Socceroos Tete Yengi, anasema timu hiyo haina wasiwasi kuhusu mwanzo wao wa polepole kwenye michezo. Kampeni ya Kombe la Dunia ya Socceroos itaanza Jumapili alasiri [[1400 aest]] dhidi ya Turkiye mjini Vancouver.
Unaweza tazama kila mechi ya Kombe la Dunia la 2026, moja kwa moja na kipekee kwenye SBS.
Bofy hapo juu kwa taarifa kamili.





