Polisi wanachunguza ajali iliyotokea kusini-magharibi mwa Sydney usiku wakuamkia, ambayo imesababisha vifo vya watoto wawili wenye umri wa mwaka moja na miaka mitano.
Nyota wa Socceroos, Awer Mabil, anasema hashangai kwamba video inayoangazia utamaduni mbalimbali wa kikosi cha Kombe la Dunia imesambaa sana. Awer Mabil ni mmoja wao - na anasema timu hiyo ina motisha ya kuifanya Australia ijivunie.
Bunge la Seneti la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limepitisha muswada unaoruhusu kufanyika kwa kura za maoni nchini humo, hatua inayoweza kufungua njia kwa Rais Felix Tshisekedi kubadili katiba na kuwania muhula wa tatu wa urais. Kwa mujibu wa katiba ya sasa, muhula wa pili na wa mwisho wa Tshisekedi unatarajiwa kumalizika mwaka 2028. Muswada huo sasa unasubiri kuidhinishwa na Mahakama ya Katiba kabla ya kupelekwa kwa rais kutiwa saini kuwa sheria.
Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.






