Serikali ya shirikisho inatetea hatua yake kali ya uhamiaji, ambayo inaimarisha sheria kwa wanafunzi wa kimataifa na watu ambao wako nchini kwa likizo, inalenga wanao baki nchini zaidi ya muda wa viza zao na wanaohama kutoka viza moja hadi nyingine, na inawapa kipaumbele wafanyakazi wenye ujuzi katika sekta muhimu.
Jimbo la Queensland limekataa kufuata mwongozo wa serikali ya New South Wales katika kuwaruhusu madereva wenye kiasi kidogo cha bangi katika mfumo wao kuwa barabarani. Sheria ya kuondoa marufuku kwa wagonjwa wanao tumia bangi kama dawa imepitishwa ndani ya bunge la New South Wales, ikiwaruhusu madereva wenye leseni isiyo na vikwazo kuendesha gari mradi tu wamesajiliwa kama watumiaji wa dawa waliosajiliwa na wana uthibitisho wa agizo halali la daktari.
Watu watano, wakiwemo maafisa wawili wa Kitengo cha Kupambana na Wizi wa Mifugo (ASTU), wameuawa katika shambulio la watu wenye silaha katika eneo la Gotu, Kaunti ya Isiolo nchini Kenya. Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Isiolo, Isaac Sang, maafisa hao walikuwa sehemu ya kikosi kilichokuwa kikifuatilia washukiwa wa wizi wa mifugo walipovamiwa na washambuliaji wenye silaha mapema Jumatano.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.






