Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari:Wanawake watatu wenye uhusiano na kundi la ISIS kufikishwa mahakamani

Moutia Elzahed has been sentenced for refusing to stand for a judge in court

Moutia Elzahed has been sentenced for refusing to stand for a judge in court Source: AAP

Wanawake watatu wa Australia wenye uhusiano na kundi linalojiita Dola la Kiislamu (ISIS) wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa makosa ya utumwa, uhalifu dhidi ya binadamu, na mashtaka ya ugaidi, baada ya kurejea nyumbani kutoka miaka kadhaa ya kuzuiliwa katika kambi ya wakimbizi nchini Syria.


Watatu hao ni sehemu ya kundi la zaidi ya wanawake na watoto kumi na wawili waliowasili Sydney na Melbourne jana usiku (Alhamisi). Familia hizo zililakiwa uwanja wa ndege na polisi, wafuasi, na vyombo vya habari.

Serikali ya Shirikisho imefichua mipango mipya ya kuwalazimisha wauzaji nje wa gesi kuelekeza asilimia 20 ya bidhaa zao kwenye soko la nishati ya ndani. Katika juhudi za kupunguza bei na kuepuka uhaba wa muda mrefu, Waziri wa Nishati Chris Bowen anasema akiba ya gesi ya pwani ya mashariki itaona moja ya tano ya mauzo ya nje ikitengwa kwa ajili ya matumizi nchini Australia kuanzia katikati ya 2027.

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Felix Tshisekedi amedokeza juu ya uwezekano wa kuwania muhula wa tatu, na kuchelewesha uchaguzi mkuu unaotarajiwa katika muda wa miaka miwili ijayo. Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari Jumatano mjini Kinshasa, Tshisekedi alisema hajaelezea nia ya kutaka muhula wa tatu, na kuongeza lakini kuwa ikiwa watu watamtaka kuendelea, atakubali.

Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now