Serikali ya shirikisho yaendelea kukariri msimamo wake, wakuto ongeza muda wa mfumo wa JobKeeper.
Polisi mjini Hong Kong imewarushia gesi ya kutoa machozi waandamanaji wanaopinga mpango wa China wa kutaka kuweka sheria za usalama wa kitaifa.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amezindua mpango wakupiga jeki uchumi, wenye thamani ya Shilingi bilioni 53.7 za Kenya.
Ethiopia, Sudan na Egypt, zinatarajiwa kuanza tena mazungumzo kuhusu bwawa la kuzalisha umeme la Ethiopia, lililojengwa kwa gharama ya dola bilioni 4 kwenye mto Nile, linalokabiliwa na utata.
Share






