Wakati Australia iliamkia mapunguzo kwa vizuizi vya idadi ya watu wanao weza kutana pamoja, viongoji katika jamii zakidini walianza kujiandaa kuwapokea watu kumi katika sehemu za ibada.
Wakati huo huo viongozi hao wamejiandaa kuwafungia milango, mamia yawaumini ambao wanatarajia wata anza kuwasili kushiriki katika ibada.
Kufikia jumatatu, mikusanyiko yote yakidini na sehemu za ibada kote nchini Australia, zitaweza wapokea waumi 10. Katika jimbo la Magharibi Australia, kuanzia jumatatu ijayo, sehemu za ibada zitaruhusiwa kuwapokea watu 20.
Na unaweza endelea kupokea taarifa mpya kuhusu coronavirus, katika lugha yako kupitia tovuti hii: sbs.com.au/coronavirus
Share






