Chama cha upinzani cha CORD, kime kuwa kikiongoza maandamano dhidi ya makamishna wa tume ya uchaguzi ya Kenya inayo julikana kwa ufipi kama IEBC. Makamishna hao wame kabiliwa na kashfa za ufisadi na upendeleo kwa chama tawala, hali ambayo imesababisha chama cha upinzani kutokuwa na imani kwa uwezo wa tume hiyo kuandaa uchaguzi ulio huru nawa haki mwaka kesho 2017.

Wakenya wengi wanao ishi nchini Australia wame kuwa waki hofia usalama wa jamaa zao nchini Kenya, SBS Swahili ilizungumza na Mh. Isaiya Kabira, waziri wa Kenya nchini Australia ambaye alitueleza msimamo wa serikali kwa maandamano dhidi ya IEBC.

Mh. Kabiira alizungumzia pia uamuzi wa serikali ya Kenya kufunga kambi ya Umoja wa Mataifa ya Dadaab ambayo iko karibu na mpaka wa Kenya na Somalia. Serikali ya Kenya ime endelea kusisitiza kuwa walio fanya shambulizi lili sababisha maafa makubwa katika chuo cha Garissa walitoka katika kambi hiyo ya Dadaab. Hata hivyo, bado haija thibitishwa iwapo baadhi yawatu walio fanya shambulizi hilo ni wakimbizi kutoka kambi hiyo ya wakimbizi.
Share





