Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari Jumatano mjini Kinshasa, Tshisekedi alisema hajaelezea nia ya kutaka muhula wa tatu, na kuongeza lakini kuwa ikiwa watu watamtaka kuendelea, atakubali.
Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inaweka ukomo wa mihula miwili tu ya uraisi. Upinzani ndani ya taifa hilo umekuwa ukimtuhumu Tshisekedi kuwa na nia ya kuibadilisha katiba ili aendelee kutawala, ukisema hatua yoyote katika mwelekeo huo utakuwa mapinduzi ya katiba.
Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.





