Miundombinu na huduma ya uzeeni vyapewa kipaumbele katika bajeti ya taifa

Mweka hazina Josh Frydenberg nje ya jengo la Hazina mjini Canberra

Mweka hazina Josh Frydenberg nje ya jengo la Hazina mjini Canberra Source: AAP

Serikali ya shirikisho imedokeza kuwa miundombinu na huduma ya uzeeni ni sehemu yavipaumbele, kwa matumizi kabla ya bajeti ya taifa rasmi kutolewa Jumanne 11 Mei 2021.


Ila upinzani unawasiwasi kuwa mfuko wa matumizi wa serikali, ni ukarabati wa haraka tu usio na busara.

Na kwa waustralia wakongwe, bajeti hii inahusu kupunguza umri, wa wakati mapato ya mauzo ya nyumba yanaweza tumiwa, kupiga jeki hela zakustaafu. Kuna taarifa kuwa kuanzia Julai mwaka ujao wa 2022, watu wenye umri wa miaka 60 na zaidi, wataruhusiwa kutumia baadhi ya faida zao za mauzo wakati umri wa sasa ni miaka 65 na zaidi.

Mweka hazina wa taifa Josh Frydenberg amesema, mabadiliko ni muhimu kwa sababu itawapa wastaafu uhuru zaidi.Hotuba ya bajeti ya mweka hazina, inatarajiwa kuanza usiku wa Jumanne, mida ya saa moja unusu kwa masaa ya mashariki Australia.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now