Watch FIFA World Cup 2026™ LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 23 Machi 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Mvua na mafuriko ya sababisha shule kufungwa Kusini Mashariki Queensland, na onyo zatolewa katik amaeneo ya Magharibi Sydney, baada ya ongezeko ya mvua nyingi na mafuriko.


Mamkala nchini Ujerumani zinatarajiwa kurefusha tena muda wa utekelezaji wa vizuizi wakati zikikabiliwa na kuongezeka kwa maambukizi mapya ya visa vya corona.

Darzeni ya maafisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa jana waliomba kusitishwa mara moja kwa mashambulizi holela na kulenga raia katika jimbo la kaskazini mwa Ethiopia la Tigray, wakitaja pia ripoti za ubakaji na vitendo vingine vya kikatili vya manyanyaso ya ngono.

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo amewaongoza viongozi kutoka sehemu mbalimbali duniani na Watanzania kwa ujumla kumuaga aliyekuwa rais wa nchi hiyo, hayati John Pombe Magufuli. Akihutubia wakati wa shughuli ya kitaifa ya kuuaga mwili wa Magufuli katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, Rais Samia amewaondolea hofu wote wenye mashaka kuhusu uongozi wake baada ya kuapishwa kufuatia kifo hicho.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now