Watch FIFA World Cup 2026™ LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya habari 28 Machi 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Takriban idadi yawa Australia lakimoja elfu hamsini hivi karibuni wanaweza poteza ajira, wakati ruzuku yamapato yaserikali ya JobKeeper yameisa hii leo jumapili 28 Machi 2021.


Jimbo la Queensland limerekodi kesi ya tatu ya COVID-19 ndani ya jamii, wakati jeshi la polisi lina sahihisha maelezo kuhusu mkusanyiko ulio fanywa na kesi iliyo thibitishwa. Uchunguzi wa ziada wa polisi wa Qld umesema kuwa, mhusika alikuwa nawageni watano katika sherehe ndani ya nyumba, nasi watu 25 kama ilivyo ripotiwa kabla.

Kiongozi wa chama cha Labor kitaifa Anthony Albanese amesema mbunge wa jimbo la Qld Andrew Laming, lazima ajiuzulu kutoka bungeni maramoja. Mbunge huyo Bowman wa chama cha LNP amesema hatawania uchaguzi mkuu ujao, baada ya tabia isiyo faa kwa wanawake katika mitandao yakijamii.

Rais Uhuru Kenyatta, katika hotuba yake Ijumaa mchana, ameeleza Kenya imeripoti ongezeko la maambukizi ya Covid-19. Kiwango hiki ni cha juu zaidi kuliko wakati janga hilo lilipoanza. Ameamuru kusitishwa vikao vya kawaida vya bunge la Agosti, na mabunge ya kwenye kaunti za Nairobi, Machakos, Kajiado, Kiambu na Nakuru na kamati zake zote.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now