Seneta maarufu wa chama cha Greens amejiuzulu kutoka chama chake, kwa ajili yakufuatilia uhuru wa weusi.
Lidia Thorpe ni mwanasiasa kutoka jamii yawa Australia wakwanza, amekuwa akizozana na wanachama wenza kwa sababu ya kura ya maoni yakuidhinisha sauti yawa Australia wa kwanza bungeni.
Hali hiyo imejiri wakati Waziri Mkuu alitumia siku ya kwanza ya vikao vya bunge mwaka huu, kuhamasisha umoja kwa kura hiyo ya maoni.






