Je Bobi Wine atafanikiwa kumbandua Museveni madarakani?

Mabango ya wagombea wa urais wa Uganda, Bobi Wine (kushoto) Yoweri Museveni (kulia)

Mabango ya wagombea maarufu wa urais wa Uganda, Robert Kyagulanyi aka Bobi Wine (kushoto) Yoweri Museveni (kulia) Source: AFP

Yoweri Kaguta Museveni ameongoza Uganda kwa zaidi ya miaka 33, ila uongozi wake umekuwa chini ya shinikizo kubwa katika miaka ya hivi karibuni.


Robert Kyagulanyi ambaye anajulikana pia kwa jina lake la usanii Bobi Wine, amekuwa mwiba kwa uongozi wa rais Museveni, akivutia maelfu yawaganda kote aliko fanya kampeni zake zakuwania urais.

Mgombea wa urais wa Uganda Robert Kyagulanyi, anayejulikana pia kama Bobi Wine, azungumza na mashabiki katika mji wavibanda wa Kibera jijini Nairobi
Mgombea wa urais wa Uganda Robert Kyagulanyi, anayejulikana pia kama Bobi Wine, azungumza na mashabiki katika mji wavibanda wa Kibera jijini Nairobi. Source: AFP

Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wanahisi ni mapema sana kwa Bobi Wine kuwa rais wa taifa hilo la mashariki ya Afrika, na kwamba rais Museveni angali na uvutio wakutosha miongoni mwa wapiga kura wengi nje ya mji mkuu wa Kampala.

Yoweri Museveni awasalimia wafuasi wake katika uwanja wandege wa Kololo Kampala, Uganda 2016.
Yoweri Museveni awasalimia wafuasi wake katika uwanja wandege wa Kololo Kampala, Uganda 2016. Source: AP

Idhaa ya Kiswahili ya SBS ilizungumza na Bw William ambaye ni mzawa wa Uganda, kuhusu kampeni za urais za mwaka huu, pamoja na mtazamo wake kwa yale ambayo waganda watazingatia wanapo ingia katika vyumba vyakupiga kura.

Bofya hapo juu kwa taaifa kamili.  


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now