Je! ushawahi kosa kazi "kwasababu ya kiwango chako cha Kiingereza" Australia?

Dr Kaitila (kushoto) kiongozi wa jamii yawa Tanzania na Bw Mike (kulia) kiongozi wa jamii yawatu kutoka DR Congo jimboni Queensland.

Dr Kaitila (kushoto) kiongozi wa jamii yawa Tanzania na Bw Mike (kulia) kiongozi wa jamii yawatu kutoka DR Congo jimboni Queensland. Source: SBS Swahili

Idadi ya watu wenye asili ya Afrika Mashariki na Kati, inaendelea kuongezeka kila mwaka jimboni Queensland.


Baadhi ya wanachama wa jamii hizo, wame dokeza kuwa moja ya kivutio cha kuishi Queensland ni sababu ya mazingira ambayo sitofauti sana na wanako toka.

Hata hivyo, maisha jimboni humo yana changamoto zake sawa na katika majimbo mengine ya Australia. Moja ya kero kubwa ikiwa ni ugumu ambao watu kutoka jamii za Afrika Mashariki na Kati hupitia, haswa wanapo tafuta ajira baadhi yao wakiombwa kuthibitisha ustadi wakiingereza licha ya wengi wao kufanyia elimu yao hapa nchini Australia.

Viongozi wa jamii yawa Tanzania Dr Sababu Kaitila na Bw Mike Fideli wa DR Congo, walieleza SBS Swahili baadhi ya hatua ambazo wamechukua, kuwatafutia wanachama wao afueni kwa kero hiyo pamoja na changamoto zingine wanazo kabiliana nazo. Bonyeza hapo juu kwa mahojiano kamili.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service