A composite created on Tuesday, June 9, 2026, featuring a young man looking despondently at his computer, with a phishing text message purportedly from a bank displayed on the screen, illustrating online fraud and scam activity. (AAP Image/Susie Dodds) NO ARCHIVING Source: AAP / Susie Dodds/AAPIMAGE
Waaustralia wanapoteza mamia ya mamilioni ya dola kutokana na matapeli, huku matapeli wakizidi kutumia akili mnemba kuwadanganya waathiriwa wao.
Wiki hii ya Uelewa wa Ulaghai, wataalamu katika uwanja huu wanachangia hatua za tahadhari ambazo watu wanaweza kuchukua ili kujilinda.
Kulingana na Scamwatch, Waaustralia wamepoteza karibu dola milioni 187 kutokana na matapeli mwaka huu pekee. Ingawa takwimu hiyo ni chini ya dola milioni 23 kuliko wakati kama huo mwaka jana, wataalamu wanasema akili mnemba inafanya ulaghai kuwa mgumu kugundua.