Wahamiaji na wakimbizi mara nyingi hulaumiwa kwa ongezeko la shinikizo la gharama ya maisha. Je! kuna namna yakuvunja mzunguko huo?
Karibu nusu yawa Australia— asilimia 49, wana amini viwango vya uhamiaji viku juu sana.
Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni ya shirika la Scanlon Foundation, ambayo hupima mshikamano wa kijamii nchini Australia.
Mwandishi wa ripoti hiyo Dkt. James O'Donnell kutoka Chuo Kikuu cha Kitaifa cha Australia alisema, ingawa mitazamo yetu kuhusu athari za uhamiaji inabaki kuwa chanya kwa kiasi kikubwa, hali hii inaweza athiriwa vibaya wakati wa shida za kiuchumi.
"Watu wanapokuwa na wasiwasi kuhusu uchumi na wanapopata ukosefu wa ajira, msongo wa kifedha, mitazamo yao kuhusu uhamiaji hupungua kidogo. Kuna uwezekano mkubwa wa kusema mambo kama wahamiaji huongeza bei za nyumba, au huondoa ajira," alisema.
Lakini je, imani hizi zina ukweli wowote? Na zinaathirije wahamiaji na wakimbizi?
Makala haya ya Kuelewa Chuki yana tazama jinsi taarifa potofu zinavyowalenga wahamiaji, na jinsi tunavyoweza pambana na hadithi potofu zenye madhara.






