Taarifa ya habari 1 Disemba 2020

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Mvutano wakisiasa kati ya Australia na China waendelea kutokota, huku viongozi wajamii wakikutana na viongozi wa serikali ya shirikisho.


Kampuni ya kutengeneza dawa ya Moderna imesema kwamba inataka idhini ya dharura kwa ajili ya kutumia chanjo yake dhidi ya virusi vya Corona hapa nchini Marekani na Ulaya. Hii ni baada ya chanjo hiyo kuonyesha ufanisi wa asilimia 94.

Kiongozi wa jimbo la kaskazini la Ethiopia linaloshuhudia mapigano la Tigray Debretsion Gebremichael amemwambia Waziri Mkuu Abiy Ahmed aache ukorofi na aondoe wanajeshi wake mara moja. Amemtaka Abiy kuondoa wanajeshi hao katika jimbo hilo ambalo Gebremichael anadai linaendelea kushuhudia mapigano makali licha ya serikali kutangaza ushindi siku mbili zilizopita.

Kenya imesema kwamba haijapokea ilani yoyote inayoitaka kumrudisha nyumbani balozi wake nchini Somalia kufuatia madai ya kuingilia masuala ya ndani na yale ya kisiasa ya taifa hilo. Nairobi pia ilipinga shutuma hizo ikizitaja kuwa zisizo na Ushahidi wowote. Mogadishu pia iliagiza balozi wa Kenya nchini Somalia Lucas Tumbo kurudi Nairobi.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service