Taarifa ya Habari 11 Aprili 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Wakazi katika jimbo la magharibi Australia wanahama nakupata makazi, wakati kimbunga chakitropiki Seroja kina karibia pwani ya kati ya magharibi jimboni humo.


Waheshimiwa wa Australia wame sherehekea maisha ya Prince Philip mume wa malkia wa Uingereza katika ibada ndani ya kanisa mjini Sydney. The Duke of Edinburgh alifariki usingizini Ijumaa tarehe 9 Aprili, miezi mbili kabla ya siku yake yakuzaliwa ambapo angefikisha miaka 100.

Uchunguzi kwa kifo cha msichana mwenye miaka saba katika hospitali ya Perth, utachunguza kama upendeleo wa tamaduni, au vizuizi vya lugha vilisababisha maombi ya wazazi wake kupuuzwa. Huduma ya afya ya watoto na vijana ya Magharibi Australia, imesema itachunguza kama tamaduni ya familia hiyo ilishawishi huduma waliyo pokea.

Rais Samia Suluhu Hassan ameenda nchini Uganda hii leo kwa ziara ya kikazi ya siku moja kufuatia mwaliko aliopewa na Rais Yoweri Museveni wa nchi hiyo. Rais Samia pamoja na mwenyeji wake Rais Museveni, watahudhuria hafla na kushuhudia utiaji saini wa mkataba kati ya Serikali ya Uganda na Kampuni ya Mafuta Ghafi ya Afrika Mashariki (EACOP) juu ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la kutoka Hoima nchini Uganda kwenda Tanga nchini Tanzania.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service