Taarifa ya habari 2 Januari 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Moto mubaya wa misitu katika maeneo ya Perth Hills magharibi Australia, waongezeka kwa ukubwa wa hekta elfu saba na, baadhi ya wakazi wana elezwa wamechelewa kuondoka katika maeneo husika.


Jeshi la Myanmar hii leo limetwaa madaraka katika mapinduzi ambayo hayakuwa ya umwagaji damu, na kumshikilia kiongozi wake aliyechaguliwa kwa njia ya demokrasia Aung San Suu Kyi na kutangaza hali ya hatari ya mwaka mmoja.

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Bobi Wine amewasilisha changamoto ya kisheria kwa mahakama ya juu nchini humo akiomba kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa rais wa mwezi Januari ambayo yalimpa ushindi rais wa muda mrefu Yoweri Museveni. Bobi Wine ambaye jina lake halisi ni Robert Kyagulanyi mwenye umri wa miaka 38 ameyapinga matokeo hayo na kusema anaamini kwamba ushindi wake uliibiwa.

Wizara ya Afya nchini Tanzania imesema Jumatatu haina mpango wa kupokea chanjo ya COVID-19 ambayo imekuwa ikiripotiwa kuwepo na kutumika katika mataifa mengine. Akiwa katika ofisi za wizara mjini Dodoma, Dkt Gwajima amesema dhumuni la ufafanuzi huo ni juu ya maswali kadhaa ambayo amekuwa akiyapokea kutoka kwa wanahabari kuhusu kujikinga na magonjwa ya kuambukiza na yasiyo kuwa ya kuambukiza.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service