Taarifa ya habari 20 Aprili 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Madaktari wameonya kuwa changamoto kubwa ya chanjo ya coronavirus nchini Australia kwa sasa ni pigo kwa imani ya umma.


Siku moja baada ya kuanza tena kwa safari kati ya Australia na New Zealand, mfanyakazi katika uwanja wa ndege wa Auckland amepatwa na virusi vya COVID-19. Mamlaka wa afya ya New Zealand wamesema mtu huyo, anajitenga nyumbani na juhudi zakutafuta alio kutana nao zinaendelea.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta anatarajiwa wiki hii kuunda jopo la uteuzi la makamishna wanne wa Tume ya Uchaguzi, IEBC, kujaza nafasi za makamishna wanne waliojiuzulu baada ya uchaguzi mkuu wa 2017. Tume ya uchaguzi (IEBC) hivi sasa ina makamishna watatu pekee. Ripoti ya BBI inapendekeza haja ya kuwa na makamishna wapya kwa tume hiyo kabla ya uchaguzi mkuu wa 2022.

Rais Xi Jinping wa China amesema mfumo wa utawala wa kilimwengu lazima ufanywe uwe wa usawa na uadilifu zaidi, na kwamba kanuni zinazowekwa na nchi moja ama baadhi ya mataifa haziwezi kulazimishwa kufuatwa na wengine.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya habari 20 Aprili 2021 | SBS Swahili