Taarifa ya habari 21 Februari 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Mradi wa utoaji wa chanjo za COVID-19 nchini Australia, umeanza siku moja mapema kuliko ilivyo ratibiwa mjini Sydney.


Waziri mkuu Scott Morrison amesema anataka uchunguzi unao fanywa, kwa jibu la shutma la ubakaji wa mfanyakazi wa zamani wa chama cha Liberal, ulete mageuzi ya muda mrefu yakitamaduni.

Rais wa Marekani Joe Biden ameanza msukumo wa kidiplomasia kufufua mkataba wa nyuklia wa mwaka 2015 kati ya Iran na mataifa yenye nguvu duniani. Wanaounga mkono makubaliano hayo wanasema atahitaji juhudi za muda mrefu kufanikisha, wakati wapinzani wanasema ajikite badala ya kuishinikiza Tehran kuingia makubaliano mapya na mazito zaidi.

Maafisa 27 wa Ikulu ya Sudan Kusini wamethibitihswa kuwa wameambukizwa virusi vya corona na kwa sasa wamewekwa karantini. Ateny Wek Ateny,ambaye ni msemaji wa Rais Salva Kiir, aliliambia shirika la habari la Ujerumani DPA kwamba walioambukizwa wanatumikia katika idara za ulinzi, huduma za mapishi na udereva, pamoja yeye mwenyewe msemaji wa rais.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service