Taarifa ya habari 27 Aprili 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Waziri Mkuu Scott Morrison ametetea mfumo wa Australia wa karantini ya hoteli, licha ya wito kwa wasafiri wanao rejea nchini kutoka ng'ambo wajitenge katika vifaa vyakikanda.


Serikali ya shirikisho imesimamisha safari zote za ndege za abiria kutoka India zinazo kuja Australia, hadi angalau tarehe 15 ya Mei 2021. Vizuizi vimewekwa pia kwa safari za ndege za moja kwa moja kutoka Dubai, Singapore na Kuala Lumpur. Waziri Mkuu Scott Morrison amesema idara ya maswala yakigeni na biashara DFAT, itatuma mifuko ya misaada India.

Waziri mkuu Roble anasema alisikitishwa na ghasia za usiku wa jumapili katika mji mkuu, Mogadishu, kati ya vyombo vya usalama vya serikali na vikosi vya upinzani. Aliongeza kuwa mazungumzo na kuelewana ndio njia pekee za kutatua mkwamo wao. Wapiganaji wa upinzani wakiwa na silaha kali walijiweka katika hali ya utayari, katika sehemu mbalimbali za mji mkuu wa Somalia, Mogadishu, Jumatatu.

Jenerali wa zamani wa jeshi la Burundi Cyrille Ndayirukiye ambaye alikuwa anatumikia kifungo cha maisha jela kwa shutma za kujaribu kuuangusha utawala wa hayati rais Pierre Nkurunziza wa Burundi amefariki Jumamosi. Ndayirukiye aliyehukumiwa tarehe 13 Mei 2015, aliaga dunia akiwa katika gereza la mkoa wa Gitega, katikati mwa Burundi, vyanzo vya habari nchini humo vimesema.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya habari 27 Aprili 2021 | SBS Swahili