Taarifa ya habari 27 Disemba 2020

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Jimbo la NSW limerekodi visa vipya saba vya COVID-19, wakati amri yakubaki nyumbani imerejeshwa kwa wakazi wa maeneo ya fukwe ya kaskazini ya Sydney, baada yakupewa msamaha mfupi wakati wa krismasi.


Uingereza imechapisha maelezo ya makubaliano yake finyu ya biashara na Umoja wa ulaya, siku tano tu kabla ya kutoka katika moja ya umoja mkubwa zaidi wa kibiashara Duniani, katika mabadiliko yake makubwa ulimwenguni, tangu kupotea kwa himaya.

Walinda amani watatu wa Umoja wa Mataifa kutoka Burundi wameuawa na wengine wawili wamejeruhiwa katika kile UN imekiita “shambulizi lililofanywa na wapiganaji wenye silaha wasiojulikana” Ijumaa huko Jamhuri ya Afrika ya Kati wakati nchi hiyo ikielekea katika uchaguzi mkuu Jumapili.

Uganda imesitisha kampeni zote za uchaguzi wa urais katika mji mkuu wa Kampala na wilaya nyingine 10 zenye idadi kubwa ya watu. Msemaji wa Tume ya Uchaguzi, Paul Bukenya, amesema sababu ya kufuta kampeni ni ongezeko la maambukizo ya virusi vya corona.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service