Taarifa ya habari 3 Januari 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Makumi yamaelfu yawatu wameombwa wajitenge, hofu inapo endelea kuongezeka kuhusu mlipuko wa COVID-19 unao ungwa na duka la B-W-S katika eneo la magharibi ya Sydney.


Idadi inayoongezeka ya wajumbe wa Republican wanaungana na juhudi za Rais Donald Trump za kuubatilisha uchaguzi, wakiapa kuyakataa matokeo ya uchaguzi huo wakati Bunge litakapoandaa kikao wiki ijayo cha kuhesabu kura za wajumbe maalum maarufu kama Electoral College na kuidhinisha ushindi wa Rais mteule Joe Biden.

Rais wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi ameomba maseneta waliokaribu naye kuunda kundi la maseneta na wabunge wanaoweza kumsaidia kufanya mabadiliko katika baraza la mawaziri linalotawaliwa na watu wanaomuunga mkono aliyekuwa rais wa nchi hiyo Joseph Kabila. Tshisekedi alivunja mkataba wa kugawana madaraka na Kabila, mnamo mwezi Desemba.

Watu wenye silaha wamewauwa raia 56 na kujeruhi wengine 20 katika shambulizi baya kabisa nchini Niger lililotokea siku ya Jumamosi. Taarifa iliyotolewa na waziri wa mambo ya ndani wa Niger Alkache Alhada imesema shambulizi hilo limetokea kwenye vijiji vya Tchomb-Bangou na Zaroumdareye vilivyo jirani na mpaka na kati ya nchi hiyo na Mali.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya habari 3 Januari 2021 | SBS Swahili