Taarifa ya habari 30 Machi 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Jimbo la Queensland linakabiliana na milipuko mbili tofauti ya COVID-19, inayo ungwa na wafanyakazi wa afya.


Kuanzia Jumatano 31 Machi, wafanyakazi wa hospitali ambao hawaja chanjwa, hawataweza watibu wagonjwa wenye COVID-19 chini ya itifaki mpya.

Waziri Mkuu Scott Morrison na Gavana Mkuu David Hurley mapema hii leo walishiriki katika hafla yakuapisha baraza jipya la mawaziri wa shirikisho katika nyumba ya serikali. Ujumbe mpya wa baraza lamawaziri ume anzishwa, linalo lenga usawa wa wanawake, usalama, usalama wakiuchumi pamoja na afya.

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuharakisha kesi, kuondoa kesi zisizo na msingi na za kubambikizwa ili kuondokana na idadi kubwa ya kesi ambazo Serikali inashindwa. Rais Samia ameyasema hayo Jumapili, baada ya kupokea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Takukuru Ikulu ya Chamwino, Dodoma.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now