Taarifa ya habari 4 Mei 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Jimbo la Magharibi Australia kusaidia jamii yawahindi jimboni humo kutuma msaada kwa jamaa wao nchini India, na serikali ya jimbo la NSW, kuwekeza katika teknolojia kuunda chanjo za mRNA


Sheria mpya inayowasilishwa katika bunge la jimbo ya Victoria, itazipa shule mamlaka yakuzuia wazazi ambao hufanya vurugu kuingia katika viwanja vya shule. Sheria hiyo itawaruhusu walimu wakuu wa shule, kutoa amri za usalama wa jamii, kwa wazazi hao ila, kama mzazi hatii amri hiyo, swala hilo linaweza fikishwa mahakamani.

Rais wa Marekani Joe Biden, ambaye hapo awali aliamua kuacha idadi ya wakimbizi iliyowekwa na mtangulizi wake ambayo ilikuwa ni chini sana kihistoria ya kuruhusu wakimbizi wanaoingia kila mwaka, Jumatatu alitangaza kwamba anaongeza mara nne ya idadi hiyo mwaka huu. “Ninarekebisha kiwango cha juu cha idadi ya kukubaliwa kwa wakimbizi kuingia ya kila mwaka ya Marekani hadi 62,500 kwa mwaka huu wa fedha," rais Biden alisema katika taarifa Jumatatu alasiri.

Hali ya wasiwasi imeendelea kuongezeka mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kufuatia mashambulizi mabaya ya Jumamosi, ambapo, wapiganaji waliwaua watu wasiopungua 19, wakiwemo wanajeshi 10, katika uvamizi wa vijiji viwili. Mashambulizi hayo yalifanyika saa chache baada ya Rais Felix Tshisekedi kutangaza hali ya tahadhari na kuzingirwa kwa majimbo mawili, na maafisa wa usalama.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service