Taarifa ya Habari 8 Mei 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Viongozi wa vyama viwili vikuu vyakisiasa nchini, wakabiliana katika mjadala wakitaifa masaa machache kabla kura za kwanza za uchaguzi mkuu kupigwa.


Chama tawala cha mseto kimeadhimisha siku yakina mama, kwa kutoa ahadi ya uchaguzi inayo lenga wazazi watarajiwa ambao wana magonjwa sugu saratani ikijumuishwa. Naye Kiongozi wa upinzani Anthony Albanese amehamisha mwelekeo wake wa kampeni ya uchaguzi, kwa kulenga haki ya malipo ya wanawake, katika hatua inayo fuata ya sera kwa ajili yakuwavutia wapiga kura.

Viongozi wa jamii zawa Afrika nchini Australia, wahamasisha chama kitakacho unda serikali mpya, kishughulikie malalamishi ya baadhi ya wanachama wa jamii yawa Afrika wanao dai wanabaguliwa kazini, wengi wao wakinyimwa kazi licha yakuwa na vyetu na uzoefu wakutosha kutekeleza majukumu ya ajira husika.

Benki kuu ya Uganda inatafakari kutoa sarafu ya kidigitali, na haijapiga marufuku sarafu ya kimtandao “cryptocurrencies” lakini ina wasiwasi kuhusu madhara ya kiteknolojia ikiwemo kumlinda mteja, na uhalifu wa kifedha amesema afisa mwandamizi wa benki kuu ya Uganda, Ijumaa.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 8 Mei 2022 | SBS Swahili