Taarifa ya habari 9 Mei 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili


Serikali imetangaza uwekezaji wa angalau dola bilioni 10 kwa huduma ya uzeeni ila, wanaharakati wanawasiwasi kuwa kupitia kupungua kwa uhamiaji, sekta hiyo haitakuwa na wafanyakazi wakutosha.

Mshukiwa wakuunga mkono kundi la wanamgambo wa daesh amerejeshwa Australia, baada yakuishi kwa miaka kadhaa nchini Syria na Uturuki. Mohamed Zuhbi mwenye umri wa miaka 30, alifikishwa mahakamani kupitia mitambo ya video mapema hii leo, kabla akabiliane na mashtaka kadhaa yakitaifa, yanayo jumuisha kuwasajili wapiganaji wakigeni kujiunga na shirika hilo lakigaidi.

Mahakama ya Uhalifu wa Kimataifa, ICC Alhamisi imemhukumu Dominic Ongwen, raia wa Uganda, ambaye zamani alikuwa kamanda wa kundi maarufu la waasi la Lord Resistance Army (LRA), kifungo cha miaka 25 jela, kwa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu. Dominic Ongwen, mwenye umri wa miaka 45, alipatikana na hatia mwezi Februari 2021, kwa mashtaka 61, yakiwa ni pamoja na mauaji, ubakaji na utumwa wa kijinsia, mwanzoni mwa miaka ya 2000, chini ya LRA, wakati huo likiongozwa na Joseph Kony, ambaye alitoweka, na hajulikani aliko.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now