Chama cha Greens kinatoa wito wa mageuzi ambayo kisheria yatahitaji kampuni zama wasiliano kama Telstra, Optus na Vodafone kutoa huduma ya kuaminika kwa wateja.
Uchunguzi ulisikia kwamba Telstra haikuchukua hatua kwa maonyo ya mara kwa mara ili kurekebisha tatizo hilo na seva ya Itifaki ya Muda wa Mtandao. Seneta wa Greens Sarah Hanson-Young anasema watoa huduma wanahitaji kuwajibika kwa kupotea kwa huduma kwa siku zijazo.
Kenya ilifunga jana kwa muda tovuti ya urais wa nchi hiyo, baada ya kile vyombo vya habari vya nchini humo kuripoti kuwa kulikuwa na shambulio la mtandao lililoambatana na madai ya fidia. Kwa mujibu wa ripoti hizo, wadukuzi walibadilisha ukurasa wa mwanzo wa tovuti hiyo na kuweka ujumbe uliokuwa ukimkosoa Rais William Ruto.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.





