Utawala wa Trump umeongeza ushuru kwa mauzo ya nje ya Australia kutoka asilimia 10 hadi 12.5, huku kiwango kipya kikianza kutumika alasiri ya leo Ijumaa.
Sikiliza makala yetu yaliyo rekodiwa hapa
Waaustralia wanatarajiwa kujibu maswali 66 yanayo wahusu wao wenyewe na hali yao ya makazi katika wiki chache tu [[Agosti 11]] huku Ofisi ya Takwimu ya Australia ikijiandaa kuanzisha Sensa ya 2026. A-B-S hufanya utafiti huo kila baada ya miaka mitano na kwa kiasi kikubwa utakamilika mtandaoni mwaka huu.
Shirika la afya la Umoja wa Afrika (Africa CDC) linaiomba Marekani kuondoa vikwazo vya usafiri dhidi ya Uganda. Hakuna visa vipya vilivyorekodiwa nchini Uganda tangu Juni 21, na mgonjwa wa mwisho aliruhusiwa kutoka hospitalini wiki iliyopita. Kulingana na Africa CDC , kuiweka Uganda kwenye orodha ya nchi zilizoathiriwa haikubaliki tena.
Hata hivyo, Washington iliongeza muda wa wasafiri kutoka Uganda kuzuiwa Julai 13 kwa siku zingine 30. Jean Kaseya, katika barua kwa Waziri wa Afya wa Marekani, anaona hatua hii kuwa isiyo sawa.
Bofya hapo juu kwa taarifa zaidi.






