Ujumbe wa kwanza wa aina yake umetumwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kufuatilia utekelezaji wa usitishaji mapigano kati ya jeshi la serikali na kundi la waasi la M23, linaloungwa mkono na Rwanda.
Ujumbe huo umewasili mjini Minembwe, jimboni Kivu Kusini, eneo ambalo limekumbwa na mapigano makali katika miezi ya karibuni.
Tume mpya ya rais inayochunguza wahusika wa ghasia zilizotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 nchini Tanzania imeanza rasmi kazi, ikiahidi kuwabaini waliopanga, kufadhili na kuratibu matukio hayo. Katika mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Mstaafu Shabani Ally Lila, amesema tume imepewa hadidu tano za rejea.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.






