Kifurushi cha mageuzi ya sheria kitawasilishwa katika Bunge la Shirikisho leo, ili kuweka mipaka ya kisheria kwa silaha za Australia na kuweka vikwazo kwa pesa za umma, uwekezaji na biashara zinazotumika kuunga mkono mauaji ya kimbari, uhalifu wa kivita, uhalifu dhidi ya ubinadamu na uvamizi haramu.
Sikiliza makala yetu yaliyo rekodiwa hapa
Muswada wa 'Mistari Nyekundu' unawasilishwa katika bunge zote mbili na Dkt. Sophie Scamps pamoja na Seneta David Pocock, kwa usaidizi wa Maseneta Lidia Thorpe, Mehreen Faruqi, Fatima Payman na Andrew Wilkie. Kundi hilo la wabunge linataka Serikali ya Albanese, iweke mipaka katika usambazaji wa silaha kwa washirika, ikiwa ni pamoja na Israeli, ikitaja vitendo vyake huko Gaza.
Rais wa Zanzibar Hussein Mwinyi amezindua Kamati ya Pamoja ya Majadiliano kati ya vyama vya CCM na ACT-Wazalendo, uteuzi huo wa wajumbe 10 unaashiria hatua mpya katika mchakato wa maridhiano ya kisiasa Zanzibar.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.






