Mfanyabiashara mmoja wa duka mjini Melbourne amefariki baada ya kushambuliwa alipokuwa akijaribu kuzuia kundi la vijana walio kuwa waki iba dukani.
Polisi wanasema Van Viet Truong mwenye umri wa miaka 60 ali enda kumsaidia mfanyakazi mwingine wa rejareja wakati wa tukio, katika kitongoji cha Sunshine magharibi mwa Melbourne siku ya Jumamosi. Alipelekwa hospitalini akiwa katika hali mbaya lakini alifariki jana alasiri.
Kiongozi wa chama cha upinzani nchini Tanzania, Chadema, Tundu Lissu, anatarajiwa kurejea mahakamani Jumatatu ya wiki ijayo kuendelea na kesi ya mashtaka ya uhaini baada ya kuwa imesimama kwa miezi kadhaa. Kesi yake ilisimama kusikilizwa mwezi Machi mwaka huu baada ya upande wa mashtaka kukata rufaa kupinga uamuzi wa mahakama kuu ambayo ilikataa ombi la serikali kutaka mmoja wa mashahidi kutoa Ushahidi wa ziada.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.






