Waziri Mkuu Anthony Albanese, amesisitiza kujitolea kwa chama chake kupunguza shinikizo la gharama la maisha katika mkutano wa kitaifa wa chama tawala.
Shirika linalo wakilisha wazazi jimboni Victoria linahimiza Chama cha Elimu cha Australia na serikali ya jimbo kufikia makubaliano kuhusu mazungumzo marefu ya mishahara, huku maelfu ya walimu wakigoma mjini Melbourne. Katika barua pepe kwa wanachama, shirika hilo linasema jamii za shule zimechoka na kutokuwa na uhakika, likitaka makubaliano ambayo yanathamini ipasavyo elimu ya umma kupitia mishahara ya ushindani na mzigo wa kazi unaoweza kudhibitiwa.
Mahakama ya Paris imethibitisha siku ya Ijumaa usiku kuamkia Jumamosi kifungo cha miaka 27 jela dhidi ya daktari wa zamani wa Rwanda Eugène Rwamucyo, ambaye alikuwa akishtakiwa tena kwa kuhusika kwake katika mauaji ya kimbari ya Watutsi nchini Rwanda mwaka 1994, chanzo cha mahakama kimesema siku ya Jumatatu.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.






